Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia Kifo cha Malkia Elizabeth II (96) wa Uingereza aliyefariki tarehe 08 Septemba, 2022 nchini Uskochi. Mhe. Rais Samia alisaini Kitabu hicho katika Makazi ya Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Oysterbay Jijini Dar es Salaam tarehe 09 Septemba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania David Concar mara baada ya kusaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia Kifo cha Malkia Elizabeth II (96) wa Uingereza aliyefariki tarehe 08 Septemba, 2022 nchini Uskochi.Friday, September 09, 2022
NUKTA AFRIKA,UNESCO YATAJA FAIDA YA WANAHABARI KUJIFUNZA
AUDIOMACK YAZINDUA 'NGOMA JUA YA NGOMA' KUKUZA UBUNIFU, MUZIKI WA KITANZANIA
KAMPUNI ya Audiomack imezindua kampeni inayojulikana “Ngoma Juu Ya Ngoma” inayolenga kukuza ubunifu na kuuza muziki wa Kitanzania na itashirikisha wasanii wakubwa wakiwemo Zuchu, Lava Lava, Jux, Barnaba na wengine.
Kampeni itahusisha Bango, ushirikiano wa Radio na, matangazo ya kidijitali, chapa ya mabasi, ushiriki wa watu wenye ushawishi na orodha za kucheza.
Katika kukuza uelewa juu ya kampeni hiyo Audiomack ilifanya Warsha Katika jiji la Dar es Salaam hivi karibuni.
Kampeni hiyo pia itahusisha mfululizo wa kwanza wamuziki wa kimataifa wa Audiomack, SKYLINE, mfululizo wamaonyesho unaohusisha matukio yaliiyotajwa hapo juu, na utaonyesha tamaduni kutoka Tanzania nakuziweka katika ubora wa juu zaidi ambao maudhui ya Audiomack yanajulikana nayo.
Audio mack pia imeshirikiana na kituo cha redio cha msanii Diamond Platnumz kilichoshinda tuzoz a Tanzania Wasafi FM kuzindua ‘Audiomack Top 10’.
Kipindi hicho kinachorushwa Ijumaa, kinaundwa na chati za Audiomack Top 10 Tanzania zinazoangazia nyimbo kubwa zaidin chini.
WADAU WA ELIMU WAWEKA BAYANA UMUHIMU WA MAKTABA MAADHIMISHO SIKU YA USOMAJI
Wednesday, February 09, 2022
Rais Wa Benki Ya AADB Ahaidi Neema Kwa Tanzania
Na Peter Haule na Saidina Msangi, WFM, Dodoma
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kuahidi kutekeleza miradi mipya katika sekta mbalimbali ikiwemo ya kilimo na pia kuwawezesha Wanawake na Vijana kiuchumi pamoja na ahadi aliyoitoa ya kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Reli ya Kisasa-SGR
Dkt. Nchemba ametoa shukrani hizo Jijini Dodoma, alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Benki hiyo, Dkt. Akinwumi Adesina, akiwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula.
Alisema kuwa Benki hiyo imetoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara za mzunguko za jijini Dodoma pamoja na ujenzi wa Uwanja wa Kimataifa wa Msalato utakaojengwa mkoani Dodoma, miradi itakayochochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Amemshukuru Rais huyo wa Benki ya AfDB kwa nia ya kusaidia miradi mingine mipya kama ya Uwezeshaji wa Wanawake na vijana lakini pia uwezeshaji katika sekta kuu za uzalishaji ikiwemo sekta ya kilimo.
Amesema maeneo hayo ni muhimu katika kukuza uchumi na yanamatokeo chanya si tu kwa watanzania lakini pia kwa Bara la Afrika kwa kuwa mradi kama wa Reli utazinufaisha nchi Jirani kwa kuwa Tanzania ina lango la Bahari hivyo miundombinu hiyo itasaidia katika kuchochea uchumi wa nchi hizo Jirani na nyingine.
Naye Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula ameipongeza Benki hiyo kwa utendaji kazi mahili chini ya Rais Dkt. Akinwumi Adesina, kwa kuwa mwaka 2021 ilitunukiwa tuzo kwa kuwa Benki Bora Duniani katika masuala ya Fedha na pia ameshukuru kwa nia ya kusaidia utekelezaji wa miradi mipya ambayo itawasaidia watanzania.
Kwa upande wake Rais wa AfDB, Dkt. Akinwumi Adesina alisema kuwa Benki yake inatambua umahili wa Tanzania katika kusimamia sera za kifedha na kiuchumi na kuahidi kuwa Benki yake itaendelea kuchangia maendeleo yake katika Nyanja mbalmbai ikiwemo miundombinu ya nishati na barabara, kilimo, uhifadhi wa mazingira, pamoja na kuendeleza sekta binafsi.
Dkt. Adesina alisema kuwa uwekezaji wa Benki yake katika miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi hapa nchini umefikia dola za kimarekani bilioni 2.5 na kwamba Benki yake iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mipya hususani katika sekta ya kilimo ili nchi iweze kuzalisha chakula kwa wingi na kukiongezea thamani kupitia maeneo maalumu ya uwekezaji.
Mkutano huo umehudhuriwa pia na Katibu Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Bw. Emmanuel Tutuba, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo kwa baadhi ya nchi za Afrika, Bw. Amos Cheptoo pamoja na Kaimu Meneja wa Benki hiyo nchini Tanzania, Dkt. Jacob Oduor, ambapo kesho, Mheshimiwa Dkt. Akinumwi anatarajia kukutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Zungu Apitishwa Kugombea Unaibu Spika
Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wamempitisha Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu kuwa mgombea wa nafasi ya Naibu Spika wa Bunge, jijini Dodoma, Jumanne Februari 8, 2022.
Zungu amepitishwa na wabunge wote wa CCM baada ya Kamati Kuu ya chama hicho kupitisha jina lake pekee kati ya wabunge 11 wa chama hicho waliokuwa wakiomba kuteuliwa kugombea nafasi hiyo.