Friday, September 09, 2022

AUDIOMACK YAZINDUA 'NGOMA JUA YA NGOMA' KUKUZA UBUNIFU, MUZIKI WA KITANZANIA

 KAMPUNI  ya Audiomack imezindua kampeni inayojulikana  “Ngoma Juu Ya Ngoma” inayolenga kukuza ubunifu na kuuza muziki wa Kitanzania na itashirikisha wasanii wakubwa wakiwemo Zuchu, Lava Lava, Jux, Barnaba na wengine.

Kampeni itahusisha Bango, ushirikiano wa Radio na, matangazo ya kidijitali, chapa ya mabasi, ushiriki wa watu wenye ushawishi na orodha za kucheza.

Katika kukuza uelewa juu ya kampeni hiyo Audiomack  ilifanya Warsha Katika jiji la Dar es Salaam hivi karibuni.

Kampeni hiyo pia itahusisha mfululizo wa kwanza wamuziki wa kimataifa wa Audiomack, SKYLINE, mfululizo wamaonyesho unaohusisha matukio yaliiyotajwa hapo juu,  na utaonyesha tamaduni kutoka Tanzania nakuziweka katika ubora wa juu zaidi ambao maudhui  ya Audiomack yanajulikana nayo.

Audio mack pia imeshirikiana na kituo cha redio cha msanii Diamond Platnumz kilichoshinda tuzoz a Tanzania Wasafi FM kuzindua ‘Audiomack Top 10’.

Kipindi hicho kinachorushwa Ijumaa, kinaundwa na chati za Audiomack Top 10 Tanzania zinazoangazia nyimbo kubwa zaidin chini.


0 komentar:

Post a Comment