Friday, September 09, 2022

Rais Samia Asaini Kitabu Cha Maombolezo Kifo Cha Malkia Elizabeth II Wa Uingereza, Oysterbay Jijini Dar Es Salaam

 




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia Kifo cha Malkia Elizabeth II (96) wa Uingereza aliyefariki tarehe 08 Septemba, 2022 nchini Uskochi. Mhe. Rais Samia alisaini Kitabu hicho katika Makazi ya Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Oysterbay Jijini Dar es Salaam tarehe 09 Septemba, 2022.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania David Concar mara baada ya kusaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia Kifo cha Malkia Elizabeth II (96) wa Uingereza aliyefariki tarehe 08 Septemba, 2022 nchini Uskochi.

0 komentar:

Post a Comment